Yanga - Local

Gamondi azipigia hesabu CBE, SC Villa

Joel JJ By Joel JJ
21 Aug 2024
Gamondi azipigia hesabu CBE, SC Villa

Wakati Yanga ikitarajiwa kukamilisha mechi ya pili hatua ya awali ligi ya mabingwa dhidi ya Vital'o siku ya Jumamosi, kocha mkuu wa mabingwa hao wa Tanzania Bara Miguel Gamondi ameanza kuipigia hesabu mechi ya raundi ya kwanza kwani kikosi chake kina asilimia kubwa ya kuiondoa Vital'o

Yanga iko mbele kwa mabao 4-0 ushindi wa ugenini waliopata katika mechi ya kwanza dhidi ya Vital'o. Ni muujiza pekee ambao wanahitaji Vital'o kupindua matokeo dimba la Mkapa wakihitaji kushinda mabao 5-0 ili kusonga mbele

Baada ya CBE kuruhusiwa na CAF kutumia uwanja wao wa nyumbani, kama timu hiyo itaitoa SC Villa, watakutana na Yanga katika hatua inayofuata ambapo mechi ya kwanza Yanga itaanzia ugenini na kumalizia nyumbani

Jumamosi CBE na SC Villa zitachuana katika mchezo wa marudiano utakaopigwa Adis Ababa huku CBE wakiwa mbele kwa mabao 2-1 ushindi waliopata nchini Uganda

Gamondi anatarajiwa kutuma mtaalam kutoka benchi lake la ufundi ili kwenda kushuhudia mchezo huo na kuwasoma wapinzani wake hao

Wakati SC Villa wakirejea katika michuano ya Kimataifa baada ya kupotea kwa miaka mingi, CBE ni mara yao ya kwanza kushiriki mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kuchukua ubingwa wa kwao kwa mara ya kwanza tangu ianzishwe 1982.

Timu hiyo imeshiriki mara mbili mashindano ya Afrika ambapo mara mbili ikicheza Kombe la Shirikisho Afrika na kutolewa hatua ya mtoano miaka ya 2005 na 2010 kabla ya msimu huu kuja kutanua historia yao kwa kucheza ligi ya mabingwa

Gamondi amekuwa na utaratibu wa kuwasoma wapinzani wake kabla ya kukutana nao na mara nyingi huenda mwenyewe uwanjani kushuhudia mechi zao

Lakini mechi za mkondo wa pili kati ya Yanga dhidi ya Vital'o na CBE dhidi ya SC Villa zote zitapigwa Jumamosi

More Stories

BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
1h ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
1h ago
READ MORE →
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
2h ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
3h ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
3h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
3h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
3h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
5h ago
READ MORE →
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
15h ago
READ MORE →
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
15h ago
READ MORE →