Stars dimbani dhidi ya Ethiopia leo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 4th September 2024


Stars dimbani dhidi ya Ethiopia leo

Saa 1 usiku timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' itashuka uwanja wa Benjamin Mkapa kuikabili Ethiopia katika mchezo wa kuwania kufuzu michuano ya Afcon 2025 itakayofanyika Morocco

Stars haipaswi kupoteza alama katika uwanja wa nyumbani ili kuwa na nafasi nzuri ya kufuzu

Kama waandalizi wenza wa Afcon 2027, ni muhimu kwa Tanzania kufuzu Afcon 2025 ili kutumia michuano hiyo kama sehemu ya uzoefu

Kaimu kocha mkuu wa Stars Hemed Morocco amesema wamepata muda mzuri wa maandalizi na matumaini ya kushinda mchezo huo ni makubwa

Morocco amewataka mashabiki wa soka nchini kujitokeza kwa wingi dimba la Benjamin Mkapa ili kuwapa hamasa wachezaji wao

Kila la kheri Stars..


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.