Saa 1 usiku timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' itashuka uwanja wa Benjamin Mkapa kuikabili Ethiopia katika mchezo wa kuwania kufuzu michuano ya Afcon 2025 itakayofanyika Morocco
Stars haipaswi kupoteza alama katika uwanja wa nyumbani ili kuwa na nafasi nzuri ya kufuzu
Kama waandalizi wenza wa Afcon 2027, ni muhimu kwa Tanzania kufuzu Afcon 2025 ili kutumia michuano hiyo kama sehemu ya uzoefu
Kaimu kocha mkuu wa Stars Hemed Morocco amesema wamepata muda mzuri wa maandalizi na matumaini ya kushinda mchezo huo ni makubwa
Morocco amewataka mashabiki wa soka nchini kujitokeza kwa wingi dimba la Benjamin Mkapa ili kuwapa hamasa wachezaji wao
Kila la kheri Stars..



