Simba - Singida- Local - Transfer

Mwenda aridhia kurejea Singida BS kwa masharti

Joel JJ By Joel JJ
4 Sep 2024
Mwenda aridhia kurejea Singida BS kwa masharti

Baba mzazi wa mchezaji Israel Mwenda amesema kijana wake yuko tayari kurejea kuitumikia Singida Black Stars kama klabu hiyo itatimiza masharti ya mkataba na kulipa fedha ambazo hawakukamilisha

Juzi Singida BS ilitangaza kumtaka Mwenda aripoti kambini au la afuate taratibu za kuvunja mkataba alioingia na timu hiyo ambapo klabu ilimtaka alipe Tsh Milioni 500

Hata hivyo Mwenda akaweka msimamo kuwa Singida BS hawakufuata makubaliano na ameanza mchakato wa kuvunja mkataba wa miaka miwili ambayo alisaini akitokea klabu ya Simba

Baba mzazi wa mchezaji huyo, Mzee Patrick Mwenda amesema kijana wake ameridhia kurejea kambini kama atamaliziwa fedha anazodai

"Wakitulipa leo, kesho kijana ataenda Singida. Maana sisi hatuna tatizo na timu, shida ya Tanzania uswahili ni mwingi. Sisi hicho hatuwezi kukikubali lazima kijana alipwe fedha yote halafu aende."

"Kijana alipaswa kulipwa milioni 340 kama signing on fee ni tofauti na mishahara yake ya kawaida. Signing on fee hii imegawanywa, kwamba malipo ya awali atalipwa milioni 200 na msimu wa pili atalipwa milioni 70 na msimu wa 3 milioni 70"

"Lakini taarifa ya klabu ya Singida ilisema milioni 200 tu. Maana watanzania wengi walikuwa wameshaamini kwamba kama kijana ameshalipwa milioni 140, hiyo 60 angemaliziwa baadae," alisema Mwenda

Katika milioni 200 ambazo Mwenda alipaswa kulipwa katika msimu wa kwanza, alipokea Milioni 140 tu hivyo anadai Tsh Milioni 60

Singida BS imethibitisha fedha hiyo italipwa lakini kwa kuzingatia makubaliano ya kimkataba, kampuni inayomsimamia mchezaji huyo ndio iliyochukua jukumu la kulipa kwa makubaliano ya kulipwa fedha hizo na Singida BS baadae

More Stories

Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
5h ago
READ MORE →
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
6h ago
READ MORE →
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
8h ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
8h ago
READ MORE →
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
9h ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
9h ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
9h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
9h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
10h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
12h ago
READ MORE →