Mjumbe wa Bodi ya Wakurugenzi klabu ya Simba Crescentius Magori amesema kiungo Yusuph Kagoma yuko huru kuitumikia Simba kwa sababu klabu haijawahi kupokea barua yoyote kutoka TFF juu ya mchezaji huyo kusimamishwa kama ilivyodai taarifa iliyotolewa na Mwanasheria wa Yanga mapema leo
Aidha Magori ameitaka TFF imuadhibu Mwanasheria wa Yanga Simon Patrick kwa kuzungumzia kesi ambayo iko mbele ya Kamati ya Sheria na Hadhi za wachezaji
Magori ameikumbussha TFF iliwahi kumuadhibu marehemu Zacharia Hans Pope wakati wa sakata la usajili wa mchezaji Bernard Morrison baada ya kuzungumza na wanahabari kuhusu kesi iliyokuwa mbele ya Kamati
"Yusuf Kagoma, Kiungo wa boli, cheza mpira, hivi vya leo ni vituko na viroja TFF chukueni hatua. Marehemu Hans Pope aliwahi kuadhibiwa kwa kuzungumza suala lililopo kwenye Kamati ya Sheria. Tunaomba hili pia litendeke"
"Simba haijawahi kupata barua yoyote ya Kagoma kusimamishwa. Tunaomba adhabu itolewe kwa aliyesema huu uongo hadharani, "aliandika Magori katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii
Kagoma yuko na kikosi cha Simba Libya kwa ajili ya mchezo wa kombe la Shirikisho dhidi ya Al Ahly Tripoli utakaopigwa Jumapili



