Mchezo wa mkondo wa pili kuwania tiketi ya kutinga hatua ya makundi ligi ya mabingwa barani Afrika kati ya Yanga dhidi ya CBE SA ya Ethiopia utapigwa Jumamosi, Septemba 21 katika uwanja wa New Amaan Complex
Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga Ali Kamwe amesema ni wakati wa mashabiki wao wa visiwani Zanzibar kupata burudani ya michuano ya ligi ya mabingwa huku akitamba wanakwenda kufuzu hatua ya makundi kwa kuibuka na ushindi mnono
Yanga ilirejea jana kutoka Ethiopia ambako walishinda bao 1-0 bao pekee lililofungwa n Prince Dube
Katika mchezo wa marudiano Yanga itahitaji ushindi au matokeo yoyote ya sare kutinga makundi kwa msimu wa pili mfululizo




