Kocha Simba afurahia suluhu Libya

Joel JJ By Joel JJ β€’ 16th September 2024


Kocha Simba afurahia suluhu Libya

Kocha Mkuu wa Simba Fadlu Davids amewapongeza wachezaji wake kwa nidhamu waliyoionyesha katika mchezo wa mkondo wa kwanza kuwania tiketi ya kutinga hatua ya makundi kombe la Shirikisho dhidi ya Al Ahly Tripoli

Mchezo huo uliopigwa dimba la Tripoli International jana, ulimalizika kwa matokeo ya suluhu ya bila kufungana, Simba ikifanikiwa kuondoka na 'cleensheet' ugenini

"Nawapongeza wachezaji wangu kwa nidhamu ya mchezo walioonyesha leo. Tumedhihirisha kwa kiasi gani tunaweza kuwa bora tukicheza bila ya mpira"

"Tulitengeneza nafasi kubwa za kufunga katika kipindi cha kwanza, mechi kubwa za aina hii hupati nafasi nyingi hivyo ni muhimu kutumia nafasi chache zinazopatikana, bahati haikuwa upande wetu"

"Ilikuwa ni mechi ya kimkakati zaidi ambayo naona tumefanikiwa kwani hatukuruhusu bao ugenini"

"Mashabiki wa Al Ahly Tripoli walifanya mazingira ya mchezo huu kuwa magumu, nawapongeza kwa kujaza uwanja lakini naamini mashabiki wa Simba watafanya zaidi"

"Waje kwa wingi watuunge mkono katika mchezo wa marudiano, tuna nafasi ya kumaliza mchezo huu nyumbani," alisema fadlu

Simba inahitaji ushindi wa aina yoyote katika uwanja wa Benjamin Mkapa ili kutinga hatua ya makundi


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.