Yanga - Local

Gamondi anataka makundi CAF CL

Joel JJ By Joel JJ
β€’
19 Sep 2024
Gamondi anataka makundi CAF CL

Licha ya ushindi wa bao 1-0 ambao Yanga walipata ugenini dhidi ya CBE SA katika mchezo wa mkondo wa kwanza kuwania tiketi ya kufuzu hatua ya makundi ligi ya mabingwa barani Afrika, Kocha Mkuu wa Yanga Miguel Gamondi amesema bado hawajafuzu hatua ya makundi hivyo wanahitaji kushinda mchezo wa marudiano

Katika makaratasi, CBE SA wanaonekana kama mpinzani mwepesi hasa baada ya kupoteza mchezo wa mkondo wa kwanza uliopigwa Ethiopia. Gamondi hawachukulii katika wepesi huo

"Mimi naheshimu kila mpinzani ninaekutana nae katika michuano hii. Tangu mwanzo wakati tunakwenda Ethiopia nilisema hatutakuwa na mchezo mwepesi na hicho ndicho kilichotokea licha ya ushindi tuliopata"

"Tuna faida ya ushindi wa ugenini lakini haina maana tayari tumefuzu, tunapaswa kupambana katika mchezo wa pili tuweze kupata ushindi na kujihakikishia nafasi hiyo"

"CBE ni timu nzuri, tulipocheza nao mwanzo hatukuwa tukiwafahamu vyema lakini sasa tunawajua, mchezo wa pili utakuwa tofauti na tutacheza mbele mashabiki wetu ambao naamini watakuja kwa wingi kutuunga mkono" 

"Licha ya kushinda, sote hatukufurahia kile kilichotokea Ethiopia, ilitakiwa kushinda kwa kiwango kikubwa lakini mambo haya yanatokea kwenye soka, ninachofurahia kila mchezaji anajutia"

"Tumefanya mazoezi ya kutosha ya kufunga mabao, naweza kusema kila kilichofanywa na washambuliaji na wachezaji wa nafasi zingine kimenivutia sana naamini tutakwenda kuwa na dakika 90 nzuri nyumbani," alisema

Uwanja wa New Amaan Complex unaochukua takribani mashabiki 15,000 uko tayari kwa mchezo huo utakaopigwa saa 2:30 usiku

Meneja wa Yanga Walter Harrison amesema wameamua kupeleka burudani ya michuano ya CAF kwa mashabiki wao wa Zanzibar ambao kama Watanzania wanastahili kupata burudani hiyo

"Zanzibar ni sehemu ya Tanzania na tuna mashabiki wengi sana hakuna mtu mwenye shaka na hilo, tulifanya tathmini ya kina na tukaona ni sehemu sahihi ya kwenda kucheza mchezo wetu wa raundi ya kwanza Ligi ya Mabingwa Afrika ambao Mungu akijaalia tutaingia kwenye hatua ya makundi," alisema

More Stories

Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
1h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
1h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
2h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
5h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
8h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
9h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
10h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
10h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
11h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
12h ago
READ MORE β†’