Simba - Local

Tumpe muda Mutale - Ahmed

Joel JJ By Joel JJ
β€’
20 Sep 2024
Tumpe muda Mutale - Ahmed

Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya Simba Ahmed Ali amesema winga Mzambia Joshua Mutale anahitaji muda kuwadhihirishia Wanasimba ubora wake

Kwa siku za karibuni, Mutale amekumbana na ukosoaji kutoka kwa mashabiki wa Simba wengi wakiamini anahitaji kubadilika kwani aina yake ya uchezaji haisaidii Simba

Hata baada ya mchezo wa mkondo wa kwanza kuwania tiketi ya kutinga hatua ya makundi kombe la Shirikisho dhidi ya Al Ahli Tripoli uliopigwa Libya, Mutale hakuwa katika kiwango bora hivyo kumlazimu kocha Fadlu Davids kumtoa katika kipindi cha pili

Ahmed amesema nyota huyo ameyasikia maoni ya Wanasimba lakini ni wazi bado ni mapema kumkatia tamaa, atahitaji muda ili kudhihirisha kwa nini Simba ilifunga safari Zambia kumsajili

"Ni kweli Joshua Mutale mchezo ulimpalia kabisa na hata ukiangalia kipindi cha pili alipata nafasi na kushindwa kuitumia baada ya hapo ilimuondoa mchezoni kwa dakika zote 90"

"Si hivyo tu kitu ambacho anachofanya Mutale bado Wanasimba hawajaridhika kutokana na ubora wake. Watu wanaufahamu ubora wa Mutale tuna matarajio nae bado ni mechi chache tumpe muda atakuwa sawa na tutafurahia matunda yake," alisema Ahmed katika mahojiano na Crown Media

More Stories

Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
1h ago
READ MORE β†’
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
11h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
12h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
12h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
16h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
19h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
20h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
20h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
21h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
21h ago
READ MORE β†’