Miamba watatu wa Ulaya wanataka kumsajili Mason Greenwood, PSG wanavutiwa na mshambuliaji wa Newcastle na Chelsea wanataka kumuuza Axel Disasi. Barcelona, Atletico Madrid na Bayern Munich ni miongoni mwa vilabu vinavyomhitaji mshambuliaji wa Marseille Mwingereza Mason Greenwood, 22. (Talksport)
PSG wanamtaka mshambuliaji wa Newcastle raia wa Uswidi Alexander Isak huku Magpies ikiweka thamani ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 kuwa takriban euro 100m (£83.8m) (Fichajes - in Spanish)
Chelsea wanataka kumuuza mlinzi wa Ufaransa Axel Disasi mwenye umri wa miaka 26 katika dirisha la uhamisho la Januari. (Fichajes - in Spanish)
Nottingham Forest inawafuatilia wachezaji wawili wa kimataifa wa Uturuki, winga wa Galatasaray Baris Alper Yilmaz, 24, na mshambuliaji wa Besiktas Semih Kilicsoy, 19. (HITC)
Arsenal walikutana na mshambuliaji wa Uingereza Ivan Toney, 28, kisha Brentford, majira ya kuchipua - lakini waliamua kutomsajili. Badala yake, alikwenda kwa klabu ya Saudi Al-Ahli. (TBR Football)
Juventus watatafuta kumsajili mshambuliaji wa Lille wa Canada Jonathan David mwenye umri wa miaka 24 mnamo mwezi Januari kwa mkataba wa euro 15m (£12.5m). (Calciomercato - In Italian)
Real Madrid inafikiria kufikia kiwango cha euro 45m (£37.7m), kipengele cha lazima katika suala la kumuuza beki wa Valencia mwenye umri wa miaka 19 kutoka Uhispania Yarek Gasiorowski. (AS – in Spanish)
Everton itampa mshambuliaji wa Uingereza Dominic Calvert-Lewin fursa ya mwisho ya kusaini mkataba mpya kabla ya mkataba wake kumalizika msimu ujao wa joto, huku Newcastle wakionyesha nia ya kumtaka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 27. (Teamtalk)
Mazungumzo ya mkataba kati ya Southampton na mlinzi wa England Kyle Walker-Peters yamegonga mwamba huku mkataba wa sasa wa mchezaji huyo wa miaka 27 ukikamilika msimu ujao wa joto. (Fabrizio Romano)
Southampton wamemjumuisha meneja wa Blackburn John Eustace kwenye orodha yao huku Saints wakifikiria nani wa kuchukua nafasi za Russell Martin. (Football Insider)
BBC



