Simba imetambulisha usajili wa winga Mcongomni Elie Mpanzu aliyetua kutoka klabu ya AS Vita
Lilikuwa ni suala la muda Simba kuthibitisha usajili wa nyota huyo ambaye wiki iliyopita alikuwepo nchini kushuhudia mchezo wa kombe la Shirikisho la CAF kati ya Simba dhidi ya Al Ahly Tripoli
Ujio wa Mpanzu wa unakwenda kuimarisha eneo la safu ya ushambuliaji ya Simba kwani anaweza kutumika kama winga au namba 10
Mpanzu ataanza kujifua mapema na Simba huku akisubiri kufunguliwa kwa Dirisha dogo la usajili Disemba 15 aanze kutumika rasmi kwenye ligi
Nyota huyo amepewa mkataba wa miaka miwili



