Transfer - International

Tetesi za usajili Ulaya, Alhamisi Oktoba 03 2024

Joel JJ By Joel JJ
β€’
3 Oct 2024
Tetesi za usajili Ulaya, Alhamisi Oktoba 03 2024

Arsenal, Bayern Munich, Manchester City na Real Madrid wako mbioni kumsajili kiungo wa kati wa Ujerumani Florian Wirtz kutoka Bayer Leverkusen msimu ujao, huku klabu hiyo ya Bundesliga ikitaka €150m (£125m) kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21. (Bild – in Deutsch)

Mkufunzi wa Newcastle United Eddie Howe na meneja wa zamani wa Chelsea Graham Potter ni wawili kati ya wachezaji wanaowania kuchukua nafasi ya Erik ten Hag iwapo ataondoka Manchester United, huku meneja wa zamani wa England Gareth Southgate na mkufunzi wa Inter Milan Simone Inzaghi pia wakiwa kwenye mfumo. (TeamTalks)

Lakini, ripoti kutoka Italia zinasema kuwa meneja wa zamani wa Juventus Massimiliano Allegri anapendelewa na Sir Alex Ferguson kuwa meneja ajaye wa Manchester United. (Express)

Meneja wa Southampton Russell Martin yuko kwenye hatari kubwa ya kupoteza kibarua chake kufuatia timu yake kuanza vibaya msimu huu. (Mirror)

Meneja wa zamani wa Chelsea Frank Lampard amedokeza nia yake ya kuwa meneja wa England, ambayo kwa sasa inashikiliwa na meneja wa muda Lee Carsley. (Football London)

Kiungo wa kati wa Real Sociedad na Uhispania Martin Zubimendi, 25, anasema hajutii baada ya kukataa kuhamia Liverpool katika dirisha la usajili la kiangazi. (Mirror)

Winga wa Borussia Dortmund, 22, Karim Adeyemi analengwa na Liverpool. Klabu hiyo ya Merseyside inamtaka mshambuliaji huyo wa Ujerumani kuchukua nafasi ya Mohamed Salah msimu ujao. (Sun)

Everton hawana wasiwasi kuhusu mpango wa dirisha la uhamisho wa Januari kutoka kwa wapinzani wao Liverpool kumnunua beki wa kati wa Uingereza Jarrad Branthwaite, 22. (Liverpool Echo)

Everton wanaweza kufufua nia yao ya kumnunua fowadi wa Paraguay Miguel Almiron, 30, ambaye huenda akaondoka Newcastle United mwezi Januari. (TeamTalks)

Manchester United wanaweza kuchagua kuongeza muda wa mwaka mmoja kwa beki wa Uingereza Harry Maguire, 31, ambaye anafikia kikomo mwishoni mwa kampeni za 2024-25, kwani wanataka kumzuia kuondoka akiwa huru. (Football Insider)

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’