NBC PL: Yanga, Azam Fc viwanjani leo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 3rd October 2024


NBC PL: Yanga, Azam Fc viwanjani leo

Ligi Kuu Tanzania Bara inaendelea kushika kasi, huku leo viwanja vitatu vikitarajiwa kuwaka moto

Bingwa mtetezi Yanga itakuwa uwanja Azam Complex, Dar es Salaam kuikaribisha Pamba Jiji. Yanga ipo nafasi ya 4 katika msimamo wa Ligi Kuu ikiwa na pointi 9 baada ya michezo 4 wakati Pamba Jiji inashika nafasi ya 14 ikiwa pointi 4 baada ya michezo 6

Huko Lindi, Azam itakuwa mgeni wa Namungo kwenye uwanja wa Majaliwa ulipo Ruangwa

Azam inashika nafasi ya 5 ikiwa na pointi 9 baada ya michezo 6 wakati Namungo ipo nafasi ya 11 ikiwa na pointi 6 baada ya michezo 5

Eneo la Mwenge, Dar es Salaam litakuwa na hekaheka wakati wenyeji KMC itakapoikaribisha Kagera Sugar kwenye uwanja wake wa KMC Complex

Katika msimamo wa ligi KMC ipo nafasi ya 12 ikiwa na pointi 5 baada ya michezo 6 wakati Kagera Sugar ni ya 15 ikiwa na pointi 4.


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.