Simba - Local

Kibu hana hofu na usajili wa Mpanzu Simba

Joel JJ By Joel JJ
β€’
3 Oct 2024
Kibu hana hofu na usajili wa Mpanzu Simba

Kiungo mshambuliaji wa Simba Kibu Denis amemkaribisha winga mpya wa timu hiyo Elie Mpanzu ambaye juzi usiku Simba ilithibitisha kukamilisha usajili wake kwa mkataba wa miaka miwili akitokea klabu ya AS Vita

Kibu amesema ujio wa Mpanzu utaongeza ubora katika safu ya ushambuliaji kwani kocha Fadlu Davids atakuwa na wigo mpana wa wachezaji wa kuwatumia katika eneo la winga

Hata hivyo amesema ataendelea kupambana katika kiwanja cha mazoezi ili kuhakikisha anampa kocha sababu ya kuendelea kumtumia

"Namkaribisha sqana Mpanzu Simba, nafahamu ni mchezaji mzuri ambaye ataongeza kitu katika timu yetu"

"Binafsi napenda ushindani kwani utafanya niongezee bidii ya mazoezi ili kumshawishi kocha kuendelea kuniamini kunipa nafasi ya kucheza"

"Hata ningeletewa Cristiano Ronaldo wa Al Nassr, bado ningefurahia kucheza naye, kwani ubora wake ungenifanya kutamani kujifunza vitu vya kunifanya kocha aone umuhimu wangu kikosini," alisema Kibu

Baada ya usajili wa Mpanzu, katika eneo la washambuliaji wa pembeni, Simba sasa itakuwa na machaguo zaidi Mpanzu akiungana na Kibu, Ladark Chasambi, Saleh Karabaka, Edwin Balua na Joshua Mutale

Kibu, Mutale na Balua ndio waliopata nafasi zaidi ya kucheza katika kikosi cha kwanza cha Fadlu

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
47m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’