Yanga - Local - Transfer

Yanga kurudi sokoni kusaka kiungo

Joel JJ By Joel JJ
4 Oct 2024
Yanga kurudi sokoni kusaka kiungo

Klabu ya Yanga iko katika mchakato wa kunasa saini ya kiungo mkabaji mpya, Charve Onoya, kutoka AS Maniema ya nchini DR Congo

Habari kutoka ndani ya Yanga zinasema mchezaji huyo ni mmoja ya watakaovaa uzi wa kijani na njano kipindi cha dirisha dogo la usajili litakalofunguliwa Desemba, mwaka huu na Januari, mwakani

Yanga inataka huduma ya mchezaji huyo kwa ajili ya kuimarisha eneo lao la kiungo, ambalo kwa sasa linaongozwa na Mganda Khalid Aucho na Aziz Andambwile

Kiungo huyo nusura ajiunge na Yanga mwanzoni mwa msimu huu, lakini dili lilifeli, na safari hii mabosi wa klabu hiyo wamerejea kwa nguvu zote

"Kwa sasa tegemeo ni Aucho, na anaonekana amechoka kutokana na kucheza michezo mingi, anahitaji msaidizi, Mudathir yeye anapewa kazi ya kwenda kushambulia mianya inayoachwa na wapinzani, mara chache anakuja kumsaidia. Andambwile bado hana uzoefu, tuna michuano mingi migumu ya kimataifa, kwa hiyo lazina tupate kiungo mkabaji mzuri na mwenye uzoefu, tumeangukia kwa huyo jamaa Mkongomani," kilisema chanzo kutoka Yanga

More Stories

Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
Wamebaki wababe wawili tu wasiofungika Ligi Kuu
4h ago
READ MORE →
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
Afcon haiwezi kuondoka Tanzania, Kenya na Uganda : Motsepe
4h ago
READ MORE →
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
7h ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
7h ago
READ MORE →
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
8h ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
8h ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
8h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
8h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
9h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
10h ago
READ MORE →