Droo ya makundi ya michuano ya kombe la Shirikisho barani Afrika (CAF CC) imefanyika Misri leo ambapo Simba imepangwa kundi A pamoja na timu za CS Cfaxien (Tunisia), CS Constantine (Algeria) na Bravos ya Angola
Novemba 28 Simba itacheza mechi ya kwanza ya makundi nyumbanii dhidi ya Bravos na kisha kusafiri Algeria kuikabili CS Constantine Disemba 08
Disemba 15 Simba itakuwa nyumbani kuikabili CS Sfaxien na kisha kusafiri Tunisia kurudiana na CS Sfaxien Januari 5
Januari 12 Simba itasafiri Angola kurudiana na Bravos na kisha kumaliza mechi ya mwisho hatua ya makundi nyumbani dhidi ya CS Constantine Januari 19
Hapa utaratibu ni uleule alama zote 9 za nyumbani lazima zibaki kisha kusaka angalau alama 2 tu ugenini kujihakikishia tiketi ya kutinga robo fainali