Yanga kuanza na Al Hilal makundi

Joel JJ By Joel JJ β€’ 7th October 2024


Yanga kuanza na Al Hilal makundi

Mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi ligi ya mabingwa barani Afrika (CAF CL) utapigwa Novemba 26 ambapo Yanga iliyopangwa kundi A, itaikaribisha Al Hilal katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa

Disemba 06 Yanga itakuwa Algeria kuchuana na MC Alger katika mchezo wa pili na kisha kuelekea DR Congo kuikabili TP Mazembe Disemba 13

Januari 03 Yanga itakuwa nyumbani uwanja wa Benjamin Mkapa kurudiana na TP Mazembe na kisha kusafiri Mauritius kumalizana na Al Hilal Januari 10

Januari 17 Yanga itahitimisha hatua ya makundi nyumbani kwa mchezo dhidi ya MC Alger utakaopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa

Ili kukamilisha mkakati wa kutinga robo fainali, Yanga itazihitaji alama zote 9 za nyumbani pamoja na kusaka angalau ushindi wa mechi moja ugenini

Hata hivyo katika misimu ya hivi karibuni Yanga imejipambanua ni timu inayoweza kushinda popote iwe nyumbani au ugenini


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.