Mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi ligi ya mabingwa barani Afrika (CAF CL) utapigwa Novemba 26 ambapo Yanga iliyopangwa kundi A, itaikaribisha Al Hilal katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa
Disemba 06 Yanga itakuwa Algeria kuchuana na MC Alger katika mchezo wa pili na kisha kuelekea DR Congo kuikabili TP Mazembe Disemba 13
Januari 03 Yanga itakuwa nyumbani uwanja wa Benjamin Mkapa kurudiana na TP Mazembe na kisha kusafiri Mauritius kumalizana na Al Hilal Januari 10
Januari 17 Yanga itahitimisha hatua ya makundi nyumbani kwa mchezo dhidi ya MC Alger utakaopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa
Ili kukamilisha mkakati wa kutinga robo fainali, Yanga itazihitaji alama zote 9 za nyumbani pamoja na kusaka angalau ushindi wa mechi moja ugenini
Hata hivyo katika misimu ya hivi karibuni Yanga imejipambanua ni timu inayoweza kushinda popote iwe nyumbani au ugenini



