Stars yatua Kinshasa kuikabili DR Congo

Joel JJ By Joel JJ β€’ 9th October 2024


Stars yatua Kinshasa kuikabili DR Congo

Timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' imewasili Kinshasa, DR Congo tayari kwa mchezo wa kuwania tiketi ya kufuzu fainali za Afcon 2025

Stars inayoshika nafasi ya pili kundi H ikikusanya alama nne, itashuka dimbani Pentecost Martyrs kesho Alhamisi katika mchezo dhidi ya DR Congo ambao utapigwa saa 1 usiku

Ni mechi muhimu kwa Tanzania kupata ushindi au hata alama moja ugenini ili kuweka hai matumaini ya kufuzu Afcon

Timu hizo zitarudiana tena wiki ijayo jijini Dar es salaam katika mchezo mwingine ambao unaweza kutoa taswira ya mwelekeo wa kundi H


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.