Transfer - International

Tetesi za usajili Ulaya, Jumamosi Oktoba 12 2024

Joel JJ By Joel JJ
β€’
12 Oct 2024
Tetesi za usajili Ulaya, Jumamosi Oktoba 12 2024

Arsenal wanapanga kuwasilisha dau la kumnunua beki wa kushoto wa Bournemouth na Hungary Milos Kerkez, mwenye umri wa miaka 20, na winga wa Cherries Antoine Semenyo mwenye umri wa miaka 24, mchezaji wa kimataifa wa Ghana. (CaughtOffside)

Mkufunzi wa Newcastle Eddie Howe, mwenye umri wa miaka 46, hana mpango wa kuondoka katika klabu hiyo licha ya kuwa miongoni mwa watu walioorodheshwa kwa ajili ya kazi ya kuinoa England ambayo iko wazi. (Telegraph - subscription required)

Kiungo wa kati wa England Kobbie Mainoo, mwenye umri wa miaka 19, anakaribia kukubali mkataba mpya katika klabu ya Manchester United. (Manchester Evening News)

Barcelona na Real Madrid zina nia ya kumsaini beki wa kushoto wa Uhispania Alvaro Fernandez, 21, ambaye Manchester United ilimuuza Benfica msimu uliopita. (Mirror)

Kiungo wa kati wa Manchester United na Denmark Christian Eriksen, mwenye umri wa miaka 32, anatarajiwa kujiunga tena na klabu yake ya zamani Ajax wakati mkataba wake utakapomalizika msimu ujao. (Sun)

Beki wa zamani wa Liverpool na taifa la Kameruni Joel Matip, 33, anafikiria kustaafu. (Ruhr Nachrichten S04 on X - in German), external)

Everton wamejiwekea malengo ya kumsajili winga wa Stuttgart na Jamuhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, Silas Mvumpa, mwenye umri wa miaka 26, mwezi Januari. (Football Insider)

Kocha wa zamani wa Manchester United Ole Gunnar Solskjaer, mwenye umri wa miaka 51, anafanya mazungumzo na "klabu kubwa" kuhusu kurejea katika kazi ya umeneja baada ya kukataa mazungumzo zaidi kuhusu kuionoa timu ya taifa ya Denmark. (Tipsbladet - in Danish), external)

Liverpool wamepangia kumchukua beki wa kati wa Palmeiras Vitor Reis, mwenye umri wa miaka 18, kama mchezaji wanayeweza kumsajili kwa siku za zijazo. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Brazil ana kifungu cha kuvunja mkataba cha pauni milioni 84. (Football Insider)

Klabu ya River Plate ya Argentina inataka kuongeza muda wa mkopo wa mshambuliaji wa Manchester City. Echeverri mzaliwa wa Argentina, mwenye umri wa miaka 18, alisaini mkataba na City mnamo Januari 2024 kwa makubaliano kwamba angesalia katika River Plate kabla ya kuhamia Uingereza mnamo Januari 2025. (TYC Sports - in Spanish)

River Plate wanataka kuongeza muda wa mkopo wa mshambuliaji wa Manchester City Claudio Echeverri. Echeverri mzaliwa wa Argentina, mwenye umri wa miaka 18, alisaini mkataba na City mnamo Januari 2024 kwa makubaliano kwamba angesalia katika River Plate kabla ya kuhamia Uingereza mnamo Januari 2025. (TYC Sports - in Spanish)

BBC

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
1h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
2h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
3h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
5h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
18h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
19h ago
READ MORE β†’