Yanga - Simba - Azam - Singida - Local

Stars yasaka ushindi dhidi ya DR Congo leo

Joel JJ By Joel JJ
β€’
15 Oct 2024
Stars yasaka ushindi dhidi ya DR Congo leo

Timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' leo inashuka uwanja wa Benjamin Mkapa kumenyana na DR Congo katika mchezo wa kuwania kufuzu michuano ya Afcon 2025

Katika kuhakikisha timu inapata sapoti kubwa ya mashabiki, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dk Samia Suluhu Hassan amenunua tiketi 20,000 za Mzunguuko kwa ajili ya mashabiki kuingia bure. Mapema Azam TV na Wadhamini wengine walilipia tiketi 10,000

Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Mh Gerson Msigwa amewataka Watanzania kujitokeza kwa wingi uwanja wa Benjamin Mkapa leo kuipa hamasa timu yao ya Taifa katika mchezo ambao Tanzania inahitaji ushindi

Ili kuweka hai matumaini ya kufuzu Afcon 2025, Stars inahitaji kushinda mchezo dhidi ya DR Congo leo

Itakuwa mechi ngumu kwa sababu DR Congo nao wanahitaji ushindi ili kujihakikishia tiketi ya kufuzu mapema

Kaimu Kocha Mkuu wa Tanzania Hamed Morocco amesema vijana wake wako tayari kwa mchezo huo na watapambana kuhakikisha wanaibuka na ushindi

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Kassim Majaliwa atakuwa mgeni rasmi wa mchezo huo ambao pia Rais Mstaafu Awamu ya nne, Dk Jakaya Mrisho Kikwete ataushuhudia katika dimba la Mkapa

More Stories

Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
33m ago
READ MORE β†’
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
10h ago
READ MORE β†’
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
11h ago
READ MORE β†’
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
Highlights : Azam Fc 0-2 Simba
11h ago
READ MORE β†’
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
Mizizima derby pilato Herry Sasii kuwaamua Azam na Simba
14h ago
READ MORE β†’
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
18h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
18h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
19h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
20h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
20h ago
READ MORE β†’