Mabao mawili ya dakika za majeruhi yaliyofungwa na Meshack Elia yameihakikishia DR Congo kufuzu kwa fainali za Afcon 2025 baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Tanzania
Ikicheza mbele ya Rais Mstaafu Awamu ya nne Dk Jakaya Kikwete, Waziri Mkuu Mh Kassim Majaliwa na viongozi wengine waandamizi, Stars ilishindwa kufua dafu mbele ya Wacongoman hao
Stars ilikosa ubunifu katika eneo la ushambuliaji, timu ilicheza vyema eneo la ulinzi na kiungo. Hata hivyo baada ya kuzuia vizuri kwa takribani dakika 88, mashambulizi ya kushitukiza ya DR Congo katika dakika za jioni yaliigharimu Stars kupoteza mchezo huo muhimu na kuweka rehani nafasi ya kufuzu Afcon 2025
Tanzania sasa inahitaji kushinda mechi mbili zilizobaki dhidi ya Ethiopia na Guinea huku ikiomba wapinzani wake hao katika kundi H wafanye vibaya katika mechi zao



