Aziz Ki aongeza mzuka Yanga

Joel JJ By Joel JJ β€’ 17th October 2024


Aziz Ki aongeza mzuka Yanga

Jana Yanga imeendelea na mazoezi Avic Town kujiandaa na mchezo wa ligi kuu dhidi ya Simba utakaopigwa Jumamosi, Oktoba 19 katika uwanja wa Benjamin Mkapa

Kikosi cha Yanga kimeimarika zaidi kuanzia baada ya wachezaji waliokuwa na majukumu ya timu za Taifa kuripoti

Stephane Aziz Ki, Prince Dube na Duke Abuya walishiriki mazoezi sambamba na wachezaji wengine ambao waliendelea na mazoezi katika kipindi chote ambacho wenzao walikuwa timu za Taifa

Meneja wa Yanga Walter Harrison amesema wachezaji wengine ambao walikamilisha majukumu ya tiimu za Tafa juzi Jumanne, wanatarajiwa kuripoti leo

Harrison amesema ari na morali ya wachezaji wao iko juu na wanajiandaa kushinda mchezo huo


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.