Jana Yanga imeendelea na mazoezi Avic Town kujiandaa na mchezo wa ligi kuu dhidi ya Simba utakaopigwa Jumamosi, Oktoba 19 katika uwanja wa Benjamin Mkapa
Kikosi cha Yanga kimeimarika zaidi kuanzia baada ya wachezaji waliokuwa na majukumu ya timu za Taifa kuripoti
Stephane Aziz Ki, Prince Dube na Duke Abuya walishiriki mazoezi sambamba na wachezaji wengine ambao waliendelea na mazoezi katika kipindi chote ambacho wenzao walikuwa timu za Taifa
Meneja wa Yanga Walter Harrison amesema wachezaji wengine ambao walikamilisha majukumu ya tiimu za Tafa juzi Jumanne, wanatarajiwa kuripoti leo
Harrison amesema ari na morali ya wachezaji wao iko juu na wanajiandaa kushinda mchezo huo








