Klabu ya Kaizer Chiefs imemteua Cedric Kaze kuwa kocha msaidizi akiungana na kocha Nasreddine Nabi waliofanya kazi pamoja Yanga kwa misimu miwili
Inaelezwa Nabi aliwataka mabosi wake wamuajiri Kaze ili kuongeza nguvu katika benchi lake la ufundi
Akiwa na Nabi katika kikosi cha Yanga, walishinda mataji sita katika misimu miwili pamoja na kucheza fainali ya kombe la Shirikisho la CAF
Tangu atue Kaizer Chiefs, Nabi amefanikiwa kuwaongeza katika benchi lake la ufundi Kaze na Khalil Ben Youssef ambao alifanya nao kazi Yanga



