Yanga - Simba - Local

Ni Simba au Yanga kwa Mkapa leo

Joel JJ By Joel JJ
β€’
19 Oct 2024
Ni Simba au Yanga kwa Mkapa leo

Unaweza kusema leo ni siku kubwa kwa wapenzi na mashabiki wa soka Tanzania pale watani wa jadi Simba na Yanga watakapochuana katika mchezo wa ligi kuu ya NBC utakaopigwa kuanzia saa 11 jioni

Unapozungumzia mechi kubwa zaidi ya mpira wa miguu Tanzania, basi so nyingine, ni hii Kariakoo Derby inayozikutanisha timu zenye upinzani wa kihistoria

Pamoja na kuwa matokeo ya mchezo wa leo hayawezi kuamua hatma kuelekea ubingwa wa ligi kuu msimu huu, lakini timu itakayoibuka na ushindi leo itajiweka juu kwenye ushinda baina ya timu hizo msimu huu

Simba iko nafasi ya tatu katika msimamo wa ligi ikiwa na alama 13 wakati Yanga iko nafasi ya tano ikiwa na alama 12 pia ikiwa na mchezo mmoja wa kiporo

Yanga inakwenda katika mchezo huo ikiwa na rekodi ya kibabe dhidi ya watani zao, ikiwa imeshinda mechi tatu mfululizo zilizokutanisha timu hizo katika mashindano yote

Msimu uliopita Wananchi waliibuka kidedea katika mechi zote mbili za ligi dhidi ya watani zao wakishinda 5-1 na 2-1 na pia kushinda 1-0 mwezi August katika nusu fainali ya Ngao ya Jamii

Ni wazi leo Simba itakwenda dimba la Mkapa ikiwa na dhamira moja tu, kumaliza uteja na kurudisha ari yao katika kuwania taji la ligi kuu msimu huu

Vijana wa kocha Fadlu Davids wameanza vyema msimu wakishinda mechi nne za ligi na sare moja

Lakini bila shaka leo watahitaji kuwa katika ubora wao ili kuweza kuondoka na alama zote tatu dhidi ya Yanga iliyojipambanua kuwa timu bora kwa sasa Tanzania

Mchezo utapigwa saa 11 jioni

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
46m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’