Baada ya kupoteza mchezo wa ligi kuu dhidi ya watani zao Yanga, kikosi cha Simba kimetua mkoani Mbeya kwa ajili ya mchezo dhidi ya Tanzania Prisons utakaopigwa uwanja wa Sokoine kesho Jumanne
Ni mchezo mwingine mgumu kwa Wekundu hao wa Msimbazi mbele ya Prisons ambayo imetoka kupoteza mchezo dhidi ya Azam Fc
Prisons wameanza msimu kwa kusuasua wakishika nafasi ya 12 katika msimamo wa ligi wakikusanya alama 7 wakati Simba iko nafasi ya nne ikiwa na alama 13
Simba imepata alama 1 kutoka mechi mbili zilizopita hivyo watautizama mchezo huu kwa umuhimu ili kurejea katika ari ya ushindi
Wakati Simba wakikabiliana na Prisons, watani zao Yanga ambao wamebaki timu pekee ambayo haijaruhusu bao msimu huu, watakuwa Azam Complex kuikabili JKT Tanzania
Singida BS imeendelea kubaki kileleni mwa msimamo wa ligi, jana ikifikisha alama 19 baada ya ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Namungo Fc



