Kimanzi afutwa kazi Tabora United

Joel JJ By Joel JJ β€’ 21st October 2024


Kimanzi afutwa kazi Tabora United

Klabu ya Soka ya Tabora United, imetangaza kuachana na aliyekuwa Kocha wao mkuu, Francis Kimanzi pamoja na aliyekuwa msaidizi wake Yusuph Chipo

Kwa mujibu wa taarifa ya klabu hiyo, uamuzi huo umechukuliwa kutokana na mwenendo usioridhisha wa klabu hiyo tangu kuanza kwa msimu huu wa 2024/24

Tabora United inashika nafasi ya 11 katika msimamo wa ligi ikikusanya alama 8 baada ya kushinda mechi mbili na kutoka sare mechi mbili

Wafuga nyuki hao wamepoteza mechi nne katika ya nane walizocheza mpaka sasa


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.