Mshambuliaji wa Fountain Gate Selemani Mwalimu ameendelea kutakata katika ligi kuu ya NBC leo akifunga bao moja na kuihakikisha Fountain Gate kuibuka na ushindi wa mabao 3-1 katika mchezo uliopigwa Babati, Manyara
Mwalimu ndiye kinara wa mabao ligi kuu ya NBC akiwa amefunga mabao sita

Mabao mengine ya Fountain Gate yalifungwa na Dickson Ambundo na William Edgar ambaye pia amefikisha mabao manne msimu huu
Bao la kufutia machozi kwa upande wa KMC lilifungwa na Andrew Vicent 'Chikuke'
Fountain Gate imepanda mpaka nafasi ya pili katika msimamo wa ligi baada ya kufikisha alama 16
Singida Black Stars ndio vinara wa ligi hiyo wakikusanya alama 19 baada ya kucheza mechi 7