Local,Normal News,Yanga, JKT

Ni mwendo wa rekodi kwa Gamondi Yanga

ProSports Media By ProSports Media
23 Oct 2024
Ni mwendo wa rekodi kwa Gamondi Yanga

Kocha Mkuu Yanga Miguel Gamondi amewapongeza wachezaji wake baada ya kucheza mechi 16 mfululizo za ligi bila ya kupoteza 

Jana Yanga iliichapa JKT Tanzania mabao 2-0 katika mchezo uliopigwa uwanja wa Azam Complex

Akizungumza baada ya mchezo huo Gamondi alisema sio kazi rahisi kucheza mechi 16 za ligi bila kupoteza lakini imewezekana kutokana na ubora wa wachezaji alionao

"Nawapongeza wachezaji wangu kwa ushindi wa leo (jana), tumecheza mechi 16 za ligi (tangu msimu uliopita) tumeshinda 15, sare 1 tukipata cleensheet 12 katika mechi hizo"

"Tumefanya mabadiliko ya kikosi katika baadhi ya maeneo tukiwapumzisha wachezaji waliotumika mchezo uliopita na kuwapa nafasi ambao hawakucheza dhidi ya Simba"

"Tunakabiliwa na ratiba ya mechi mfululizo ambayo inatulazimu kufanya hivyo, tutacheza Jumamosi dhidi ya Coastal Union na pia tutacheza Jumatano (ijayo) dhidi ya Singida BS"

"Tutaendelea kufanya kazi kwa bidii ili kuhakikisha tunazidi kufanya vizuri katika mechi zinazofuata," alisema Gamondi

Ni mwendo wa rekodi kwa Yanga kwani sasa Wananchi wamecheza jumla ya mechi 26 katika mashindano yote (ukiacha mechi za kirafiki) mechi 16 zikiwa za ligi kuu 

Mara ya mwisho Yanga kupoteza ni mechi ya mashindano ni 05/04/2024 dhidi ya Mamelod Sundowns mchezo wa mkondo wa pili robo fainali ya ligi ya mabingwa

Yanga walipoteza mchezo kwa mikwaju ya penati 3-2 baada ya suluhu ya bila kufungana kwa dakika 180. Hata hivyo ni mchezo ambao Mamelodi walinufaika na makosa ya kibinadanu ya Mwamuzi

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
46m ago
READ MORE →
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE →
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE →
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE →
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE →
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE →
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE →
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE →
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE →
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE →