Klabu ya Namungo Fc imemkabidhi Kocha Juma Mgunda mikoba ya kukinoa kikosi cha timu hiyo akichukua nafasi ya Mwinyi Zahera
Kulingana na taarifa iliyotolewa na Namungo Fc, Zahera ataendelea kusalia katika timu hiyo akiwa mshauri wa benchi la ufundi
Mgunda ambaye ni kocha msaidizi wa timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars', amewahi kuzinoa klabu za Coastal Union, Simba Sc huku kibarua chake cha mwisho ikiwa kuinoa Simba Queens




