Hersi ashinda tuzo Ufaransa

Joel JJ By Joel JJ • 24th October 2024


Hersi ashinda tuzo Ufaransa

Rais wa Yanga na Mwenyekiti wa Shirikisho la Vilabu Afrika (ACA) Injinia Hersi Ally Said ameshinda Tuzo ya Mwanamichezo mwenye mchango kwenye maendeleo ya mpira wa miguu barani Afrika

Sherehe za utolewaji tuzo hizo za Nigeria-France Sports Awards, zilifanyika jijini Paris, Ufaransa, juzi

Tuzo ya Injinia Hersi ilipokelewa na Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa na Mwakilishi wa Kudumu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni (UNESCO) Mhe.Ali Jabir Mwadini 


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.