Al Ahly yabeba Super Cup Misri

Joel JJ By Joel JJ β€’ 25th October 2024


Al Ahly yabeba Super Cup Misri

Ahly wamefanikiwa kutwaa taji lao la 15 la Kombe la Super Cup la Misri siku ya Alhamisi, kwa kuwashinda wapinzani wao Zamalek kwa penalti 7-6 kufuatia sare tasa katika muda wa kawaida mjini Abu Dhabi

Nahodha na kipa Mohamed El Shenawy alikuwa shujaa wa Ahly, akiokoa penalti mbili na kuhitimisha ushindi huo katika mikwaju mikali

Mashetani Wekundu walilipiza kisasi cha kushindwa kwao na Zamalek katika Kombe la Super Cup la Afrika wiki nne tu kabla, walipochapwa kwa mikwaju ya penalti na majirani zao wa Cairo

Hata hivyo, mechi hiyo ilichezwa chini ya wingu la mabishano, huku wachezaji watatu wa timu ya Zamalek wakiwekwa kizuizini Abu Dhabi siku chache kabla ya mchezo huo

Hiyo ni mara ya nne mfululizo Al Ahly wanatwaa taji hilo


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.