Jumamosi, Oktoba 26 nyasi za uwanja wa Sheikh Amri Abeid mkoani Arusha zitawaka moto pale Coastal Union watakapoumana na mabingwa wa Tanzania Yanga katika mchezo wa ligi kuu ya NBC
Coastal Union iliyohamishia makazi yake Arusha kwa muda kupisha ukarabati wa uwanja wao wa Mkwakwani, wamepania kuchafua rekodi ya Yanga ya kutopoteza mchezo wala kuruhusu bao msimu huu
Coastal Union imetangaza viingilio vya mchezo huo ambapo Majukwaa pendwa ya Mzunguuko kiingilio ni Tsh 10,000/-. Hata hivyo ili kushuhudia mchezo huo katika majukwaa mengine, mifuko ya mashabiki lazima 'itoboke' kiasi!




