Simba yaifunza soka Namungo Fc, yaichapa 3-0

Joel JJ By Joel JJ β€’ 25th October 2024


Simba yaifunza soka Namungo Fc, yaichapa 3-0

Wekundu wa Msimbazi Simba Sc wameendeleza ubabe wao katika uwanja wa KMC Complex wakiibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Namungo Fc katika mchezo wa ligi kuu ya NBC

Ulikuwa mchezo wa upande mmoja kwa muda mwingi, pengine mambo yangekuwa mabaya zaidi kwa Namungo Fc kama Simba ingetumia vyema nafasi nyingi walizotengeneza

Mabao ya Simba katika mchezo huo yalifungwa na Shomari Kapombe aliyefunga bao la mapema dakika ya 5 kabla ya Jean Charles Ahoua kuongeza la pili dakika ya 33 muda mfupi baada ya kuingia akichukua nafasi ya Awesu Awesu aliyeumia

Ahoua amefikisha mabao matatu akiwa ndiye kinara wa mabao kwa upande wa Simba akiwa pia na pasi nne za mabao

Msumari wa mwisho katika jeneza la Namungo Fc ulipigiliwa na kiungo Debora Mavambo na kuihakikishia Simba alama tatu muhimu zilizowasogeza hadi nafasi ya pili katika msimamo wa ligi

Mambo bado ni magumu kwa Namungo Fc ambayo leo imepoteza mchezo wa tatu mfululizo


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.