Yanga, Prisons, Dodoma Jiji viwanjani NBC PL

Joel JJ By Joel JJ β€’ 26th October 2024


Yanga, Prisons, Dodoma Jiji viwanjani NBC PL

Ligi Kuu ya NBC inaendelea leo kwa mechi tatu kupigwa katika viwanja mbalimbali

Baada ya kupoteza mechi mbili mfululizo katika uwanja wa nyumbani, Tanzania Prisons leo wanashuka dimba la Sokoine kuikabili KMC

Pengine ni mechi ya kuamua hatma ya kocha Mbwana Makata kwani kama Prisons itakosa ushindi leo, kibarua chake kitakuwa mashakani

Mabingwa watetezi Yanga wako ugenini mkoani Arusha katika mchezo dhidi ya Coastal Union

Mechi nyingine inayosubiriwa kwa hamu na mashabiki wa soka nchini. Yanga ndio timu pekee ambayo imeshinda mechi zote bila ya kuruhusu bao msimu huu

Coastal Union wamejipata katika mechi za karibuni, leo watakuwa dimba la Sheikh Amri Abeid wakiongozwa na kocha Juma Mwambusi kusaka alama tatu mbele ya vijana wa kocha Miguel Gamondi

Dodoma Jiji na JKT Tanzania zitahitimisha ratiba ya leo kwa mechi itakayopigwa uwanja wa Jamhuri mkoani Dodoma saa 1 usiku


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.