Bao la dakika ya 25 lililofungwa na Jean Beleke lililotosha kuihakikishia Yanga ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Coastal Union katika mchezo wa ligi kuu uliopigwa uwanja wa Sheikh Amri Abeid
Maabad Maulid alikaribia kuifungia Coastal Union bao la mapema kama sio mpira wake wa kichwa kugonga mwamba kabla ya kuokolewa na walinzi wa Yanga
Mpira wa kona uliopigwa na Maxi Nzengeli ulipelekea piga nikupige langoni kwa Coastal Union kabla ya kumfikia Baleke aliyefunga
Yanga imeandikisha ushindi wa saba ikirejea nafas ya pili katika msimamo wa ligi. Aidha wananchi wameandikisha cleansheet ya saba pia
Katika mchezo uliopigwa mapema, Prisons ilikubali kichapo cha mabao 2-1 kutoka kwa KMC nyumbani
Ni kipigo cha tatu mfululizo kwa Prisons, matokeo ambayo yanaweka mashakani kibarua cha kocha Mbwana Makata
Dodoma Jiji ikafanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya JKT Tanzania katika mchezo uliopigwa uwanja wa Jamhuri