Vurugu za mashabiki zaiponza Al Ahli Tripoli

Joel JJ By Joel JJ β€’ 27th October 2024


Vurugu za mashabiki zaiponza Al Ahli Tripoli

Shirikisho la soka barani Afrika (CAF) limeipata na hatia klabu ya Al Ahli Tripoli baada ya mashabiki wake kuwafanyia vurugu wachezaji na maafisa wa Simbaa katika mchezo wa mkondo wa kwanza kuwania kufuzu hatua ya makundi kombe la Shirikisho

Al Ahli Tripoli wamezuiwa kuingiza mashabiki katika mechi zao mbili za michuano ya CAF

Klabu hiyo pia imeipigwa faini ya kiasi ya dola 20,000 sawa na takribani Tsh. 55 millioni kutokana na vurugu zilizojitokeza uwanjani kwenye mchezo huo uliopigwa jijini Tripoli Septemba 15 na kumalizika kwa matokeo ya suluhu ya bila kufungana

Simba ilifanikiwa kutinga makundi baada ya ushindi wa mabao 3-1 katika mchezo wa marudiano uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa Septemba 22


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.