Shirikisho la soka barani Afrika (CAF) limeipata na hatia klabu ya Al Ahli Tripoli baada ya mashabiki wake kuwafanyia vurugu wachezaji na maafisa wa Simbaa katika mchezo wa mkondo wa kwanza kuwania kufuzu hatua ya makundi kombe la Shirikisho
Al Ahli Tripoli wamezuiwa kuingiza mashabiki katika mechi zao mbili za michuano ya CAF
Klabu hiyo pia imeipigwa faini ya kiasi ya dola 20,000 sawa na takribani Tsh. 55 millioni kutokana na vurugu zilizojitokeza uwanjani kwenye mchezo huo uliopigwa jijini Tripoli Septemba 15 na kumalizika kwa matokeo ya suluhu ya bila kufungana
Simba ilifanikiwa kutinga makundi baada ya ushindi wa mabao 3-1 katika mchezo wa marudiano uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa Septemba 22




