Kikosi cha timu ya soka ya Tanzania, Taifa Stars, leo saa 4:00 usiku kwa saa za Afrika Mashariki, kitajitupa kwenye Uwanja wa de la Capitale, jijini Nouakchott, nchini Mauritania kucheza mechi ya mtoano, kwa ajili ya kutafuta tiketi ya kucheza fainali za mataifa kwa wachezaji wanaocheza Ligi za ndani (CHAN). Kocha Mkuu wa timu hiyo Bakari Shime amesema wapo tayari kwa mapambano





