Vinara wa ligi kuu ya NBC Singida Black Stars tayari wako visiwani Zanzibar kuelekea mchezo wao wa ligi kuu dhidi ya Yanga ambao utapigwa Jumatano, Oktoba 30 katika uwanja wa New Amaan Complex
Kocha Mkuu wa timu hiyo Patrick Aussems amesema msimu huu wamedhamiria kufanya mabadiliko kwenye nafasi ya juu katika msimamo wa ligi
Juzi Singida BS iliichapa Fountain Gate mabao 2-0 na kujichimbia kileleni mwa msimamo wa ligi wkifikisha alama 22 alama moja mbele ya wapinzani wao Yanga
Huo ulikuwa ushindi wa 7 katika mechi 8 walizocheza mpaka sasa msimu huu
"Mwanzo mzuri kwenye ligi ni kielelezo tosha kuwa tunataka kufanya mabadiliko kwenye nafasi ya juu msimu huu"
"Tumeongoza ligi kwa kipindi kirefu, nia yetu ni kukaa pale mpaka mwisho ingawa si rahisi, lakini tunataka kule juu kuwe na mabadiliko," alisema



