Paris St-Germain wameungana na Real Madrid katika kinyang'anyiro cha kumsajili beki wa kulia wa Liverpool Mwingereza Trent Alexander-Arnold, 26. (Fichajes – In Spanish)
Liverpool, wakati huo huo, wameulizia kuhusu beki wa kulia wa RB Salzburg Bosnia na Herzegovina Amar Dedic, ambaye anatarajiwa kuchukua nafasi ya Alexander-Arnold. (Caught Offside)
Wolves wamemfanya kiungo mkabaji wa Watford na Georgia Giorgi Chakvetadze, 25, kuwa mchezaji wanayemlenga mwezi Januari. (Sun)
Rais wa Real Madrid, Florentino Perez anaandaa misingi ya nani atakayechukua nafasi ya meneja Carlo Ancelotti msimu ujao huku akimpigia debe kocha wa Bayer Leverkusen Xabi Alonso. (Sport – in Spanish)
Mshambulizi wa zamani wa Italia Mario Balotelli, 34, amefanyiwa vipimo vya matibabu siku ya umatatu kabla ya kusajiliwa na klabu ya Serie A ya Genoa. (Fabrizio Romano)
West Ham wanavutiwa na mshambuliaji wa Atalanta na Nigeria Ademola Lookman, 27, huku meneja Julen Lopetegui akitumai kuimarisha safu yake ya mashambulizi mwezi Januari. (GiveMeSport)
Manchester City wanajiandaa kumpa mlinzi wa Croatia Josko Gvardiol, 22, mkataba ulioboreshwa wenye thamani ya £150,000 kwa wiki ili kuongeza muda wake wa kukaa Etihad Stadium kwa miaka miwili hadi 2030. (Star)
Kiungo mshambuliaji wa Uingereza na Chelsea Cole Palmer, 22, bado anajitolea kwa The Blues licha ya kuhusishwa na kutaka kuondoka, ikiwa ni pamoja na kurejea Manchester City. (Football Insider)
AC Milan wana nia ya kumpa winga wa Liverpool na Italia Federico Chiesa mwenye umri wa miaka 27 njia ya kurejea Serie A. (Caught Offside)
Beki wa zamani wa Ujerumani Mats Hummels, 35, anaweza kuondoka Roma mwezi Januari licha ya kujiunga na klabu hiyo ya Serie A kama mchezaji huru msimu wa joto. (Nicolo Schira)
BBC



