Timu ya Taifa ya Tanzania inayohusisha wachezaji wa ndani, imeanza vibaya kampeni ya kuwania kufuzu fainali za CHAN 2025 ikikubali kipigo cha bao 1-0 dhidi ya Sudan katika mchezo uliopigwa huko Mauritania
Bao la dakika ya 23 lililofungwa na Mohammed Abdulrahman liliihakikishia Sudan ushindi huo wa nyumbani
Tanzania sasa itahitaji kushinda angalau mabao mawili ili kufuzu kwa michuano hiyo itakayofanyika Afrika Mashariki yaani Tanzania, Kenya na Uganda
Kama mwenyeji mwenza wa michuano hiyo, Tanzania inapaswa kupambana ili kuhakikisha inafuzu



