Nyota wa zamani wa Chelsea, Emmanuel Petit, amesema Cole Palmer bado hajafikia kwenye ubora wa viwango vya dunia licha ya kufanya vizuri katika kikosi cha The Blues kwa kipindi cha miezi 12
Petit, ambaye alichezea Chelsea mara 76 kati ya 2001 na 2004 chini ya kocha Claudio Ranieri na alikuwa pia kwenye kikosi cha Arsenal ya Arsene Wenger iliyoshinda ubingwa wa Ligi Kuu England msimu wa 1997/98, amekuwa akiifuatilia sana timu yake ya zamani, The Blues
Petit anaamini vyombo vya habari huko Uingereza vinampamba zaidi Palmer kuliko uhalisia wa ubora wake
"Anavyovumishwa Cole inaendena na kiwango chake?” alihoji Petit na kuendelea. Hapana, sidhani"
"Palmer alikuwa na msimu mzuri ule uliopita, lakini huu ameanza kwa kasi hafifu hadi hapo Septemba alipoonyesha uhai"
"Vyombo vya habari vimekuwa vikipiga kelele nyingi kuhusu vipaji vichanga vya wachezaji. Palmer ni mchezaji mzuri sana, lakini bado hajafikia viwango vya kuwa mchezaji wa dunia"
"Ameonyesha ubunifu wa kutosha, lakini bado hajafika kuwa wa kiwango cha dunia kwa sasa," alisema



