Local,Transfer News,Simba

Fadlu ataka watatu dirisha dogo

Joel JJ By Joel JJ
β€’
28 Oct 2024
Fadlu ataka watatu dirisha dogo

Licha ya kikosi chake kuonekana kuimarika, Kocha Mkuu wa Simba Fadlu Davids bado amehitaji maboresho zaidi katika usajili wa dirisha dogo linalotarajiwa kufunguliwa Disemba 16 hadi Januari 15 2025

Baada ya kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa watani zao Yanga katika mchezo wa ligi kuu uliopigwa Oktoba 19, Fadlu alidokeza kuwa lazima yafanyike maboresho katika baadhi ya maeneo ili kuwa na timu imara zaidi

Imeelezwa kuwa kocha huyo amehitaji wachezaji watatu ambao anaamini wataongeza ubora katika maeneo yenye changamoto

Tayari Simba imemsajili winga Elie Mpanzu kutoka klabu ya AS Vita ambapo mchezaji huyo anasubiri kufunguliwa kwa dirisha dogo

Mpanzu yuko nchini akiendelea kujifua na kikosi cha Simba kinachofanya mazoezi yake katika uwanja wa Mo Simba Arena

Kiungo mshambuliaji Foday Trawally raia wa Gambia, anayekipiga Klabu ya Cetinkaya TSK ya Uturuki ni jina la pili linalotajwa kuelekea Msimbazi

Simba ilifanya jitihada za kumsajili nyota huyo mwenye umri wa miaka 22 katika dirisha lililopita la usajili lakini haikuwezekana

Habari zilizopatikana kutoka ndani ya klabu hiyo, zinasema mazungumzo baina ya pande mbili yameshaanza na Simba inataka kumpa mkataba wa miaka mitatu mchezaji huyo

Chanzo kutoka ndani ya klabu hiyo kinasema kuwa Simba imeamua kuongeza kiungo mshambuliaji anayechezea klabu hiyo iliyopo Ligi Draaja la Pili nchini humo, ili kuwasaidia wachezaji wawili kwenye eneo hilo ambao ni Jean Charles Ahoua na Awesu Awesu

"Ni usajili unaotokana na matakwa ya kocha, amesema anahitaji dirisha dogo waingie wachezaji watatu wa viwango vya juu vya kimataifa kwa ajili ya mechi kubwa:

"Mchezaji huyu ni kiungo mshambiliaji, ambaye kazi yake itakuwa ni kusimama nyuma ya washambuliaji, kutengeneza nafasi na kutoa pasi za mwisho"

"Skauti yetu imejiridhisha kuwa ni mchezaji bora na anayefaa kwa kazi hiyo, kocha anahitaji kiungo anayetengeneza nafasi rahisi zaidi kwa mastraika na huyu ndiye chagua," kilisema chanzo hicho

Mbali na mchezaji huyo, habari zinasema Kocha Mkuu wa Simba, Fadlu Davids, anahitaji beki wa kati ambaye ni mrefu na mwenye nguvu kwa ajili ya michezo migumu ya kimataifa kwani anadai mabeki wake tegemeo ni wafupi, hivyo anayekuja anaweza kumsaidia kwa kiasi kikubwa kutengeneza ukuta imara zaidi

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
3h ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
3h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
4h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
5h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
5h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
6h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
7h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
20h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
20h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
21h ago
READ MORE β†’