Manchester United wametangaza kwamba hatimaye wameachana na Meneja wao Erik ten Hag baada ya kipigo cha mabao 2-1 kutoka kwa West Ham jana
Ten Hag anaondoka huku akiwaacha mashetani Wekundu wakishuka hadi nafasi ya 14 kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya Uingereza
Katika taarifa rasmi, United ilithibitisha kuondoka kwa Ten Hag na kwamba Ruud van Nistelrooy atachukua mikoba ya muda pamoja na timu ya sasa ya makocha hadi mrithi wa kudumu atakapoteuliwa
"Erik ten Hag ameacha nafasi yake kama Meneja wa kikosi cha kwanza cha Manchester United," klabu hiyo ilisema
Erik aliteuliwa Aprili 2022 na kuiongoza klabu hiyo kutwaa mataji mawili ya nyumbani, akishinda Kombe la Carabao mnamo 2023 na Kombe la FA mnamo 2024



