Bao la dakika za lala salama lililofungwa na Salum Kihimbwa limeinusuru Fountain Gate kukubali katika uwanja wake wa nyumbani huko Manyara baada ya kulazimisha sare ya mabao 2-2 dhidi ya Mashujaa Fc
Kwa upande mwingine Mashujaa Fc watajilaumu kwa kukosa ushindi katika mchezo huo ambao walitangulia mbela kwa mabao mawili
Seif Karihe aliifungia bao la kwanza Mashujaa Fc mapema tu dakika 15 na Hassan Ali akaongeza la pili dakika ya 28 na kuipa Mashujaa uongozi wa mabao 2-0 ambao ulidumu hadi dakika ya 34 pale Nicholas Gyan alipoifungia Fountain Gate bao la kwanza
Timu hizo ziliendelea kushambuliana kwa zamu Fountain Gate wakionekana kufanya majaribio mengi zaidi na hatimaye walifanikiwa kusawazisha dakika za lala salama na kufanikiwa kuondoka na alama moja
Fountain Gate wanaendelea kusalia nafasi ya tano wakiwa na alama 17 wakati Mashujaa wakiwa nafasi ya sita na alama 13





