Kihimbwa anauwasha moto ligi kuu

Joel JJ By Joel JJ β€’ 29th October 2024


Kihimbwa anauwasha moto ligi kuu

Fountain Gate imeanza vyema msimu huu ligi kuu ya NBC ikishika nafasi ya tano baada kwenye msimamo wa ligi baada ya kukusanya alama 17

Kama utazungumzia mafanikio ya Fountain Gate msimu huu basi hutakosa kutaja jina la kiungo mshambuliaji Salum Kihimbwa

Kihimbwa amehusika katika mabao saba yaliyofungwa naa timu hiyo akifunga mabao matatu na kutoa assist nne

Jana alibeba tuzo ya nyota wa mchezo dhidi ya Mashujaa Fc akifunga bao la pili la Fountain Gate katika mchezo ambao ulimalizika kwa matokeo ya sare ya mabao 2-2

Kihimbwa, Selemani Mwalimu, William Edgar na Dickson Ambundo wamekuwa chachu ya mafanikio ya kikosi cha Fountain Gate msimu huu


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.