Local,Normal News,Simba, Mashujaa

Simba yaitisha Mashujaa Fc

Joel JJ By Joel JJ
30 Oct 2024
Simba yaitisha Mashujaa Fc

Baada ya mchezo dhidi ya JKT Tanzania kuahirishwa, Wekundu wa Msimbazi, Simba Sc wameweka nguvu katika mchezo unaofuata dhidi ya Mashujaa Fc ambao utapigwa Ijumaa, Novemba 1 katika uwanja wa Lake Tanganyika

Kikosi cha Simba jana kilionekana kikifanya mazoezi katika mchana wa jua kali, ikielezwa Kocha Mkuu wa timu hiyo Fadlu Davids anawaandaa vijana wake kukabiliana na mazingira ya joto kali mkoani Kigoma hasa ikizingatiwa mchezo huo utapigwa saa 10 jioni

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba Ahmed Ali amesema timu inaandaliwa vyema ili kuhakikisha wanabeba alama zote tatu Kigoma

"Tupo kwenye maandalizi makali, na tunafanya maandalizi ya safari ili kuelekea mjini Kigoma kucheza na Mashujaa, kwa hiyo nawaambia wanachama na mashabiki wote wa Simba, baada ya kuahirishwa mchezo wetu dhidi ya JKT Tanzania, nguvu zote sasa tunaelekeza Kigoma dhidi ya Mashujaa Novemba Mosi"

"Furaha yetu imesogezwa mbele, tukutane Kigoma tukafurahi tena," alisema Ahmed

Simba imeshinda mechi zote ilizocheza ugenini msimu huu, alama tano walizopoteza ni katika mechi ambazo walikuwa nyumbani

Wekundu hao wa Msimbazi wanashika nafas ya tatu katika msimamo wa ligi wakiwa na alama 19

More Stories

BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
BREAKING: Tajiri wa Chelsea Boehly ang’atuka kwenye klabu
12m ago
READ MORE →
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
Ngorongoro Heroes yaweka malengo makubwa CECAFA U20
26m ago
READ MORE →
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
Yanga SC kukipiga mchezo wa kirafiki na St George uwanja wa Uhuru
1h ago
READ MORE →
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
Messi aongeza taji jingine, afikisha mataji 49 katika kazi yake
1h ago
READ MORE →
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
Raphinha, Yamal wampa wakati mgumu Mbappe mbio za ufungaji bora La liga
1h ago
READ MORE →
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
Manchester United yaanguka Old Trafford, yatupwa nje kwenye Carabao
1h ago
READ MORE →
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa  Yanga SC “Your next: Yanga”
SimbaSC yatuma ujumbe mzito kwa Yanga SC “Your next: Yanga”
2h ago
READ MORE →
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
Barcelona yaendeleza dozi La Liga, yaipiga Racing Santander 7-2
4h ago
READ MORE →
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
Mnyama avunja uteja Chamazi, sasa macho Dabi ya Kariakoo
14h ago
READ MORE →
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
Simba mwendo mdundo, yaichapa Azam Fc 2-0
14h ago
READ MORE →