Mechi sita za michuano ya Kombe la Carabao huko England zinapigwa leo katika viwanja tofauti
Brighton inaialika bingwa mtetezi Liverpool katika uwanja wa The American Express Community huku Crystal Palace ikiwa mgeni wa Aston Villa katika uwanja wa Villa Park
Manchester United ambayo imemtimua Erik Ten Hag hivi karibuni ni mwenyeji wa Leicester City katika uwanja wa Old Trafford
Mchezo mwingine unaosubiriwa kwa hamu ni kati ya Tottenham Hotspur na Manchester City kwenye uwanja wa Tottenham Hotspur
Arsenal itakuwa ugenini kuivaa Preston North End kwenye uwanja wa Deepdale wakati Newcastle United ni mwenyeji wa Chelsea katika uwanja wa St James' Park




