Local,Transfer News,Yanga

Yanga kuwaongeza mikataba Pacome, Yao

Joel JJ By Joel JJ
β€’
30 Oct 2024
Yanga kuwaongeza mikataba Pacome, Yao

Klabu ya Yanga imeanza mazungumzo ya kuhuisha mikataba ya nyota wake wa kikosi cha kwanza raia wa Ivory Coast Pacome Zouzoua na Yao Kouassi, imefahamika

Yao na Pacome ni miongoni mwa wachezaji katika kikosi cha Yanga ambao mikataba yao inamalizika mwishoni mwa msimu huu kama ilivyo kwa kiungo Mganda Khalid Aucho

Mapema wiki hii zilivuna tetesi kuwa klabu ya Simba inafuatilia kwa ukaribu upatikanaji wa wachezaji hao ambao ifikapo Disemba wataruhusiwa kuzungumza na timu yoyote kwa kuwa mikataba yao itakuwa chini ya miezi sita

Hata hivyo habari ya uhakika kutoka ndani ya uongozi wa Yanga ni kuwa Wananchi wamepiga hatua kubwa katika majadiliano ya kuwaongeza mikataba

Wakala wa wachezaji hao Zambro Traore tayari yuko nchini kukamilisha mazungumzo na Yanga kwa niaba ya wateja wake

Zambro anatarajiwa kushuhudia mchezo wa ligi kuu leo kati ya Singida Black Stars dhidi ya Yanga utakaopigwa uwanja wa New Amaan Stadium baadae leo

Zambro anawasimamia wachezaji wengine kama Stephane Aziz Ki na Joseph Guede ambaye kwa sasa anaitumikia Singida BS

More Stories

Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
Klopp amchagua Ter Stegen, kipa namba moja Ujerumani
44m ago
READ MORE β†’
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
Mo Dewji aichochea Simba, aweka milioni 200 dhidi ya Azam
1h ago
READ MORE β†’
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
BREAKING: Chelsea wagonga hodi PSG kwa Fabian Ruiz
1h ago
READ MORE β†’
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
Pape sakho kutoa nafasi Raja kumsajili Philipinho
2h ago
READ MORE β†’
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
Kocha De Zerbi na Tottenham Yake Mambo magumu, Watolewa kwenye Carabao Cup
3h ago
READ MORE β†’
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
Azam FC dhidi ya Simba leo, hatumwi mtoto dukani
4h ago
READ MORE β†’
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
Patrice Motsepe kuwasili Tanzania kwa ukaguzi wa maandalizi ya AFCON 2027
4h ago
READ MORE β†’
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
Alama tatu za jasho na damu kwa Yanga SC...! Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
Highlights : Yanga 1-0 Geita Gold
17h ago
READ MORE β†’
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
Hatimaye Yanga waonja uchungu wa red card baada ya Aziz Ki kuonyeshwa kadi nyekundu
18h ago
READ MORE β†’