Yanga kuwaongeza mikataba Pacome, Yao

Joel JJ By Joel JJ β€’ 30th October 2024


Yanga kuwaongeza mikataba Pacome, Yao

Klabu ya Yanga imeanza mazungumzo ya kuhuisha mikataba ya nyota wake wa kikosi cha kwanza raia wa Ivory Coast Pacome Zouzoua na Yao Kouassi, imefahamika

Yao na Pacome ni miongoni mwa wachezaji katika kikosi cha Yanga ambao mikataba yao inamalizika mwishoni mwa msimu huu kama ilivyo kwa kiungo Mganda Khalid Aucho

Mapema wiki hii zilivuna tetesi kuwa klabu ya Simba inafuatilia kwa ukaribu upatikanaji wa wachezaji hao ambao ifikapo Disemba wataruhusiwa kuzungumza na timu yoyote kwa kuwa mikataba yao itakuwa chini ya miezi sita

Hata hivyo habari ya uhakika kutoka ndani ya uongozi wa Yanga ni kuwa Wananchi wamepiga hatua kubwa katika majadiliano ya kuwaongeza mikataba

Wakala wa wachezaji hao Zambro Traore tayari yuko nchini kukamilisha mazungumzo na Yanga kwa niaba ya wateja wake

Zambro anatarajiwa kushuhudia mchezo wa ligi kuu leo kati ya Singida Black Stars dhidi ya Yanga utakaopigwa uwanja wa New Amaan Stadium baadae leo

Zambro anawasimamia wachezaji wengine kama Stephane Aziz Ki na Joseph Guede ambaye kwa sasa anaitumikia Singida BS


  

XTRA 90 INSIDER

Get the latest tactics & rumors delivered to your inbox.